Kwa Nini Upendezwe na Ujumbe wa Biblia?
Biblia ndicho kitabu ambacho kimeenezwa zaidi
ulimwenguni. Kwa nini? Kwanza, ni rahisi kuielewa. Ina habari kuhusu
watu halisi, jinsi walivyoshirikiana na pia uhusiano wao na Mungu.
Masimulizi hayo yanatufundisha mambo muhimu kwa sababu yameandikwa kwa
maneno yanayoeleweka kwa urahisi. Hivyo, Biblia imetafsiriwa katika
lugha nyingi, na watu wanaoishi eneo lolote na wakati wowote wanaweza
kuielewa. Ushauri wa Biblia unatunufaisha sikuzote.
Jambo muhimu ni kwamba, Biblia si tu kitabu kinachozungumzia habari za Mungu bali pia ni kitabu kutoka kwa
Mungu. Biblia inatujulisha jina la Mungu, utu wake, na kusudi lake
lisilobadilika la kuumba dunia na wanadamu. Pia, inaeleza kuhusu vita
kati ya wema na uovu, na jinsi mambo yatakavyokuwa mazuri wakati ujao.
Ikiwa tutasoma Biblia tukiwa na maoni mazuri, tutaimarisha imani na
tumaini letu.
Biblia ina habari ambazo hatuwezi kupata mahali pengine popote. Kwa mfano, Biblia hutueleza ukweli kuhusu mambo yafuatayo:
- Historia ya wanadamu na chanzo cha mateso
- Mpango wa Mungu wa kuwakomboa wanadamu
- Mambo ambayo Yesu ametufanyia
- Wakati ujao wa wanadamu na dunia
Kipengele: Habari mpya, Tuisome Biblia
0 Maoni