CHANGAMOTO KATIKA MAISHA YA UJANA

Unknown | 3:54:00 PM | 0 Maoni

Katika maisha ya ujana kuna changamoto mbali mbali ambazo kijana ana wajibu wa kuzishinda, basi hebu tuone
baadhi ya vijana na changamoto walizokutana nazo;
 Kijana Yususfu aliyependwa zaidi na mzee Yakobo, alichukiwa na ndugu zake hata wakapanga kumwua kwa
kuwa alipendwa zaidi na baba yao;

 “Ndugu zake wakaona ya kuwa baba yao anampenda kuliko ndugu zake wote, wakamchukia, wala hawakuweza kusema naye kwa amani.”............ 
 
Wakamwona toka mbali, na kabla hajawakaribia, wakafanya shauri juu yake ili wamwue. Wakasema wao kwa wao, Tazama, yule bwana ndoto anakuja. Haya, twende, tukamwue na kumtupa katika birika mojawapo, nasi tutasema, Mnyama mkali amemla; kisha tutaona zitakuwaje ndoto zake.” (Mwanzo 37:4, 18-20)
Kijana Yusufu alisingiziwa uovu na mke wa Potifa hata kufungwa gerezani;  “Ikawa alipoona ya kwamba amemwachilia nguo yake mkononi mwake, naye amekimbia nje, akawaita watu wa nyumbani-
mwake, akasema nao, akinena, 

 
Angalieni, ametuletea mtu Mwebrania atufanyie dhihaka. Ameingia kwangu, ili alale nami, nikalia kwa sauti kuu. Ikawa aliposikia ya kuwa nimepaza sauti yangu na kulia, aliiacha nguo yake kwangu,akakimbia, akatoka nje......... Ikawa bwana wake aliposikia maneno ya mkewe aliyomwambia, akisema, Mtumwa wako amenitenda mambo kama haya, hasira yake ikawaka. Bwana wake akamtwaa Yusufu, akamtia gerezani, mahali walipofungwa wafungwa wa mfalme, naye akawamo humo gerezani.” (Mwanzo 39:13-15, 18-20)

Katika siku za mfalme Nebukadreza, aliam uru vijana watatu, yaani Shadraka Meshaki na Abednego kutupwa katika tanuru la moto kwa kuwa waligoma kuiabudu sanamu. “
Basi Nebukadreza akatoa amri kwa hasira na ghadhabu, waletwe hao Shadraka, na Meshaki, na Abednego

 Basi wakawaleta watu hao mbele ya mfalme. Nebukadreza akajibu, akawaambia, Enyi Shadraka, na Meshaki, na Abednego, je! Ni makusudi hata hammtumikii mungu wangu wala kuisujudia sanamu ya dhahabu niliyoisimamisha?............... Basi watu hao wakafungwa, hali wamevaa suruali zao, na kanzu zao, na joho zao, na mavazi yao mengine, wakatupwa katikati ya ile tanuru iliyokuwa ikiwaka moto.” (Danieli 3:13-14, 21)

Kipengele: ,

KUHUSU NEEMA MBISE MINISTRY:
Ni Mchungaji na mwimbaji wa nyimbo za injili hapa Tanzania!

0 Maoni